STAA wa sinema za Kibongo, Ummy Wenceslaus 'Dokii' amewakemea watu wanaomsema kuwa anajipendekeza kwa Rais Jakaya Kikwete na kuwataka waache kwani yeye hajipendekezi.
Ummy Wenceslaus 'Dokii'.
Akizungumza na Kipindi cha Action & Cut cha Channel Ten hivi karibuni, Dokii alisema kutokana na jinsi alivyoshiriki katika kampeni mbalimbali za Kikwete hadi kupata ajali na kuumia mkono, wambeya wamekuwa wakimzushia kuwa alijipendekeza na hakupewa msaada wowote alipoumia.
“Nawashangaa wanaosema kuwa najipendekeza kwa JK, eti wanasema nilitelekezwa. Kwa taarifa yao tu ni kwamba, JK aliposikia nimepata ajali, alituma madaktari Wazungu kuja kunihudumia.
“Halafu hata wakisema najipendekeza pia naweza nikakubali, nisipojipendekeza kwake wanataka nikajipendekeze kwa nani? Najua hata wao wanatamani kuwa karibu na viongozi kama mimi,” alisema Dokii.
Rais mwinyi akutana na Princess Sophie wa Uingereza
-
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali
Mwinyi, ameihakikishia Uingereza kwamba Zanzibar inaendelea na mikakati na
juhudi k...
12 minutes ago
0 comments:
Post a Comment